Posted in

AFISA KILIMO MSAIDIZI DARAJA LA II (AGRICULTURAL FIELD OFFICERS) – Nafasi 292- – MDAs & LGAs – UTUMISHI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Kumb.Na.JA.9/259/01/C/5                                                                               16 Oktoba, 2025

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya na MDAs & LGAs
anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza
nafasi 17,710 kama ilivyoainishwa katika tangazo hili;

8.0 AFISA KILIMO MSAIDIZI DARAJA LA II (AGRICULTURAL FIELD OFFICERS) –
Nafasi 292

8.1 MAJUKUMU YA KAZI
• Kushirikiana na watafiti kuendesha vishamba vya majaribio,

• Kukusanya/kuhifadhi takwimu za majaribio,
• Kuwafundisha wakulima mbinu za kilimo bora,
• Kuwafikishia wakulima matokeo ya utafiti,
• Kuwafundisha wakulima mbinu bora za kilimo, matumizi ya mbolea na madawa,
pembejeo za kilimo,
• Kukusanya na kutunza takwimu za mazao na bei kwa wiki mwezi, robo na mwaka
ngazi ya halmashauri,
• Kukusanya takwimu za mvua,
• Kushiriki katika savei za kilimo,
• Kushirikiana na vikundi vya wakulima kuhusu matatizo na teknolojia sahihi za kutumia,
• Kupanga mipango ya uzalishaji,
• Kupima uotaji wa mbegu na kusimamia taratibu za ukaguzi,
• Kutathmini na kusavei maeneo ya vyanzo vya maji kwa ajili ya kuhifadhi,
• Kutunza miti mizazi

• Kuwatambua wasambazaji wa pembejeo,
• Kutoa mafunzo ya lishe kwa wakulima,
• Kufanya vipimo vya ubora, unyevunyevu na uotaji wa mbegu,
• Kusimamia taratibu za ukaguzi,
• Kudhibiti visumbufu vya mazao na mimea,
• Kusimamia shughuli za kila siku za majaribio ya kilimo,
• Kuwaelimisha wakulima juu ya matumizi bora ya udongo na maji,
• Kutoa ushauri wa kilimo mseto,
• Kuandaa sheria ndogo za hifadhi ya mazingira na
• Kutoa taaluma ya uzalishaji wa mboga, matunda, maua na viungo.
8.2 SIFA ZA MWOMBAJI
• Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha nne au Sita (VI) wenye stashahada (Diploma) ya
kilimo kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

8.3 NGAZI YA MSHAHARA
TGS.C

MASHARTI YA JUMLA
1. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania wenye umri usiozidi miaka 45 isipokuwa
kwa wale tu walioko kazini serikalini.
2. Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutumia maombi na wanapaswa
kuainisha kwenye mfumo wa kuombea ajira ulemavu walionao kwa ajili ya
taarifa kwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
3. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye
anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees)
watatu wa kuaminika.

4. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na
Mwanasheria/Wakili.
5. Waombaji kazi ambao ni waajiriwa katika Utumishi wa Umma, WASIOMBE na
wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyopo katika waraka namba
CAC45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
6. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti
vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili ambavyo ni vyeti vya kuzaliwa, kidato cha
Nne, kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho, na vyeti vya kuhitimu
mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika:-
Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
Computer Certificate

Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
7. “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati matokeo za kidato
cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
8. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na
kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU, NECTA na NACTE).
9. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba
isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
10. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi wahusika watachukuliwa hatua za
kisheria.
11. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 29 Oktoba, 2025.
12. Kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwa pamoja na vyetivya elimu, anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa;
KATIBU,
OFISI YA RAIS,
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA,
S. L. P. 2320,
Mtaa wa Mahakama, Tambukareli,
DODOMA.
13. Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal)
kupitia anuani ifuatayo; https://portal.ajira.go.tz/. (Anuani hii pia inapatikana kwenye
tovuti ya Sektretarieti ya Ajira kwa kuingia sehemu iliyoandikwa ‘Recruitment
Portal’).
14. Maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu ulioainishwa katika tangazo hili
HAYATAFIKIRIWA.

Limetolewa na:
KATIBU
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

APPLY NOW 

JOIN US TODAY

WHATSAPP GROUP 1

WHATSAPP GROUP 2

WHATSAPP GROUP 3

LINKEDIN

TELEGRAM


Discover more from Mwanampotevu Digital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *